MTUNZI gwiji wa vitabu barani Afrika, Profesa Ngugi wa Thiong'o amesema idadi ya Waafrika wanaosoma vitabu imeshuka na kutishia maendeleo ya watu barani kutokana na kutegemea kazi za waandishi wa nchi za Magharibi.Ngugi alisema hayo jana jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari baada ya ufunguzi wa Kongamano la Sita la Usomaji kwa Wote linalofanyika Chuo Kikuu cha Dar es salaam kwa siku tano.